Waigizaji Wakubwa Ambao Ni Mashoga,Kama Ulikuwa Hujui,Ndio Hawa Sasa#Teknofacts - teknomovies
Waigizaji Wakubwa Ambao Ni Mashoga,Kama Ulikuwa Hujui,Ndio Hawa Sasa#Teknofacts

Waigizaji Wakubwa Ambao Ni Mashoga,Kama Ulikuwa Hujui,Ndio Hawa Sasa#Teknofacts

Share This
Kwa wenzetu ishu ya Ushoga  (Gay) kwa sasa imeanza kuwa kawaida na bado inaendelea kuwa kawaida hasa kutokana na baadhi ya nchi kwa miaka ya karibuni kuanza kuruhusu ndoa hizo za jinsia moja kufanyika.
Mfano wa nchi hizo ni kama Uingereza,Marekani,Brazil,Scotland,Hispania,Ufaransa,Ujerumani,Kolombia,Ireland na nyingine nyingi hususani kutoka Bara la Ulaya huku kwa Afrika ni South Afrika pekee ambao wanaruhusu Ndoa za jinsia moja.

Makala hii inaangalia kwa upande wa Mastaa baadhi wa filamu ni ambao wanajihusisha na ndoa za jinsia moja yaani kwa kifupi nao ni Mashoga kama wafuatavyo;

Matt Dallas
Dallas na Hamilton
Staa huyu akitokea katika mchongo wa Kyle Xy ambao uliweza kuvuma sana katika miaka ya 2009,Mwaka 2013 alitangaza rasmi kumchumbia mpenzi wake ambae ni mwimbaji Blue Hamilton na mwaka 2015 wakaamua kufunga ndoa rasmi na kufunga rasmi seke seke Lao na mpaka sasa bado wanaishi pamoja.

Wentworth Miller
Jamaa kafahamika sana katika Series kali ya Prison Break kama Michael Scolfield,Lakini baada ya kujitangaza yeye ni shoga,hakika aliwachafua watu wengi na mpaka sasa kuna watu hawaamini kama Jamaa ni Shoga,ila ukweli ndio huo.
Jamaa alikataa mualiko aliopewa na moja ya Taasisi inayoandaa maadhimisho ya filamu huko Urusi,kutokana na nchi hiyo kukataza mambo ya Ushoga ambapo Michael aliandika Barua ya kukataa mualiko huo na kusema kuwa Hawezi kuudhuria sherehe hizo katika nchi ambayo,Mashoga kama yeye wananyimwa haki zao za msingi za kupendana na kuishi kwa Amani.

Colton Haynes
Colton Haynes na Jeff Leatham
Staa huyu wa michongo mikali kadhaa ya Series kama Arrow,Teen Wolf na filamu kama San Andreas. Jamaa kwanza ni rafiki wa Karibu wa Matt Dallas mwigizaji mwenzake ambae nae ni Shoga kama nilivyoelezea hapo juu,
Huyu tayari yupo kwenye ndoa kabisa na jamaa ambae nae ni mwigizaji akifahamika kwa jina la Jeff Leatham ambapo juzi juzi ndio wametoka kufunga ndoa yao,Oktoba 27 mwaka huu na mahusiano yao yamedumu kwa takribani miaka 4.

Charlie Carver
Huyu dogo unampata fresh sana katika Teen Wolf,The Leftover,Fist Fight,Desperate Housewives ambapo amekisanua poa sana lakini na Yeye ni mchele mchele Tu.

Huyu Jamaa mwanzoni mwa mwaka jana aliamua kujitokeza hadharani kwa kuandika katika Instagram yake kuwa yeye ni Shoga ambapo anasema kuwa imemchukua muda sana kuamua kuonesha wazi jinsi alivyo ili awe huru zaidi na watu woote waweze kujua maana ameishi na hicho kitu kwa muda mrefu sana na alikuwa akitamani kusema hadharani.

Jussie Smollet
Mkali wa Empire na pia Alien:Covenant,Baada ya kupeleka Ushoga wake katika Series ya Empire lakini Ukweli ni kuwa jamaa pia ni Shoga.

Katika mahojiano na kituo kimoja cha habari,Smollet au Jamal kama anavyofahamika sana katika mchongo wa Empire alifunguka kwa kukubali kuwa yeye ni Shoga na wala haogopi kusema kwasababu ndio ukweli huo na haihitaji mtu yoyote amwambie lolote juu ya ishu hiyo.

Jamaa ni rafiki mkubwa wa Naomi Campbell,ambapo inasemekana wamejuana tangu wakiwa wadogo mpaka kucheza pamoja katika mchongo wa Empire,Mara kadhaa walikuwa wakihusishwa kutoka pamoja lakini Baada ya mchizi kufunguka hivyo hakika alivunja kila kitu.

Luke Evans
Mkali wa michongo ya Dracula Untold,Fast n Furious 6,Clash of Titans,Beauty and The Beast Lakini huyu jamaa tangu mwaka 2002 alishakiri kuwa yeye ni Shoga.

Jimmy Parsons 
Mkali,Wa Bing Bang Theory pamoja na The Hidden Figures nae pia ni shoga ambae yupo kwenye ndoa yake ambapo May 2017 alifunga ndoa na mchumba wake Todd Spiewak.

Wapo wengi sana,Lakini wachache ndio hao,Yapi maoni yako?Utaendelea kutazama Filamu zao au utakula ngumu Tu.





No comments:

Post a Comment

Pages