YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-9 - teknomovies
YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-9

YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-9

Share This
Ilipoishia…..

Ukumbuke ni vichwa viwili tu ambavyo vilitazamwa kwa jicho la ushindani kwenye game ambao ni Tupac na Biggie Notorious. Biggie akawa amebaki mwenyewe, ingawa yeye binafsi aliona hiyo ndo time ya kung’aa kwenye ramani kwani pamoja ya kuwa na beef na Tupac lakini dunia ilikuwa inamuelewa zaidi Tupac kuliko yeye, wajibu wake uliokuwa mbele ni kuhakikisha na yeye anajenga umaarufu kama wa Tupac au pengine zaidi.

Endelea……..



Pamoja ya kuwa Harakati za muziki zilikuwa zikiendelea lakini ukweli ni kwamba kila mmoja alikuwa na wasi wasi juu ya mustakabali wa maisha yake ya mbeleni. Kila mtu hakujua nini kingefuata. Kibaya zaidi ni kwamba Biggie aliachia Diss Track kwenda kwa Tupac aliyoipa jina la “Who Shot Ya” ambapo lengo lake ni kujihami na sekeseke la kuhusishwa na mauaji hayo.


West Coast Side ilibaki na wasanii wakubwa watatu ambao ni Snoop Doggy, Easy E na Dr Dre upande huu haukua na nguvu tena kwani waliobaki wote si watu wa ma beef au watu wanaopenda figisu figisu huku Upande wa East Coast Side chini ya Record label ya Bad Boyz iliyokuwa ikimilikiwa na Puff Daddy tayari walikuwepo wakali kadhaa akiwemo Jay Z na Notorious Mwenyewe ambao hawa walikuwa wanang’aa kupita maelezo. Coverage ya media yote ikawa East Coast Side, Interview nyingi wakawa wanapewa East Coast Side. 


Maisha yakawa yanasonga lakini mke wa Biggie Faith Evans (ambae aliimbwa na Tupac kwenye wimbo wa Het Em Up) alikuwa akiogopa sana kwani baadhi ya watu walidhani aliyepanga mauaji ya Tupac ni mumewe . Hata hivyo Biggie hakuwa na kibali cha muda mrefu cha kuvuta pumzi kwenye uso wa dunia kwani miezi 6 baadae alidunguliwa na yeye kwa risasi ambazo zilichukua uhai wake.


Tukio la kupigwa risasi lilifanywa tarehe 8 march 1997 siku ambayo Biggie na yeye alikuwa akitoka kwenye party huko Petersen Automotive Museum, akiwa amekaa kiti cha mbele kabisa katika gari aina ya SUV Chevrolet ambapo mdunguaji alitegea gari isimame ili ampate vizuri. Baada ya gari kusimama mlengaji alifyatua risasi mara nne ambazo zote zilimpata Biggie Notorious. Alikimbizwa katika Hospitali ya Cedars- Sinai lakini ilipofikia saa 7: 00 usiku Biggie aliaga dunia.

Gari alilotumia Biggie mara ya mwisho na kupigwa risasi

Pamoja na Askari kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo lakini jamii ilibaki na sintofahamu, hawakuwa na majibu sahihi ya nani alitekeleza mauaji hayo. Kevin McClure ni polisi aliekuwa akisimamia shtaka hilo na mwaka 2010 alilifunga rasmi shtaka hilo kutokana na kukosekana kwa ushahidi ambao ungempata mtuhumiwa.


Itaendelea……

Usisahau Kutufollow Instagram na Twitter @Teknomovies kwa Updates mbalimbali na pia Subscribe Youtube Channel ya DM Online Tv.

Pages