YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-6 - teknomovies
YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-6

YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-6

Share This
Ilipoishia……….

Suge hakupenda label yake ishiriki kwenye mambo haya kwani walikuwa wakitumia kiasi kikubwa cha fedha kwenye misaada lakini alishindwa kumwambia Tupac juu ya suala hilo kwani yeye ndo anaeleta faida kubwa kwenye label yake sasa akimwambia si atavuruga biashara? Ikabidi avumilie tu na ashiriki kishingo upande. Kikubwa kilichomuumiza ni siku waliyotumia takribani $ 60 million kwa ajili ya msaada, hili Suge lilimuuma mno.

Endelea…………

Tupac aliskwishajua mahusiano yake na Suge hayana muda mrefu yatavunjika hii ni kwa sababu yale anayoyafanya hayampendezi mwenzake kwani Suge akili yake ilikuwa kwenye pesa tu na si kingine hivyo tupac akaamua kuanzisha record label yake ya Makaveli ambayo aliitumia  kusambaza kazi zake na baadae akamsainisha moja ya wasanii wa rap “The Outlawz”.

Wakati Tupac anaanzisha record label  , Suge alijua Makaveli Records itakuja kuwa na mafanikio, hilo lilimshtua kwani aliona kila dalili ya record label hiyo kuwa tishio upande wa West (West Coast Side). Alichokuwa anakifanya Tupac ni kuiba baadhi ya wasanii kutoka katika label ya Death Row na kuwavuta Makaveli Record na kuna nyakati Suge uvumilivu ulimshinda akawa anamchana Tupac.

Suge aliogopa umaarufu wa label ya Makaveli utamvurugia Biashara ya label yake na mwisho wa siku apotee kwenye ramani ya muziki hivyo hakukuwa na njia nyingine zaidi ya kumpoteza (kumuua) .

Ukumbuke Tupac tayari ana beef na Biggie, P Diddy katika ishu za muziki na polisi nao walikuwa hawampendi Tupac kutokana na tabia zake za awali ambazo zilikuwa si za kistaarabu hapo nyuma ingawa alibadilika lakini ndo hivyo tabia ni kama ngozi ya mwili.

Kutokana na nadharia hizo Suge alijua kabisa tukio la mauaji likifanyika basi watakaonyooshewa vidole ni wengi kwani Tupac alishajiweka kwenye mazingira ya beef na watu wengi, sasa ili asijitenge kabisa akaanza kuwa karibu na Biggie kwa kusapoti nyimbo zake lakini pia akawa karibu na polisi ili asibaki kuwa na uapnde wake bali awepo pande zote.

Tarehe 7 September 1996 siku hii kulikuwa mechi ya ndondi kati ya Mike Tyson na Bruce Seldon ambayo ilifanyika huko Las Vegas Nevada, kwa kuwa Suge alijua Tupac na Tyson ni marafiki basi kivyovyote vile ataenda kwenye mechi hiyo, hivyo na yeye akaamua aende na awe upande huo huo wa Tyson. Siku hiyo Tupac alikuwa na show kwenye club ya  Suge’s night club “662” akasita kwenda Vegas kwa ajili ya kutazama ndondi lakini baadae alikubali .


Siku hiyo pia Bodyguard wake alimwambia asibebe Bastola kwani yeye atamlinda huko Vegas na hii ilikuwa ni mara ya kwanza Bodyguard huyo kumuomba Tupac aache silaha na kweli Tupac alitii agizo hilo. Wakaenda Vegas kucheki mechi nae Suge alikuwepo na katika pambano hilo Tyson alishinda katika round ya 10. 

Wakati wanatoka katika ukumbi wa MGM Grand, Tupac aliona mtu akipora cheni kwa mmoja wa watu waliokuwepo kwenye mechi hiyo, jamaa aliyeporwa hakukubali wakaanza kuzichapa na hapo Tupac aliamua kuingilia ugomvi huo, kumbe ugomvi huo ulikuwa ukihusisha vikundi viwili kutoka West Coast Side vikundi hivyo vilijulikana kwa majina ya Crips na Bloods. Wakati hayo yote yanatokea Suge alikuwa akishuhudia kwani aliamua kufuatilia kila tukio analofanya tupac usiku huo .

Itaendelea.......... 

Usisahau kutufollow Instagram na Twitter @Teknomovies kwa Updates mbalimbali na pia Subscribe Youtube Channel ya DM Online Tv.

Pages