MFAHAMU KWA UNDANI PRODUCER S2KIZZY, KATIKA MAHOJIANO HAYA. - teknomovies
MFAHAMU KWA UNDANI PRODUCER S2KIZZY, KATIKA MAHOJIANO HAYA.

MFAHAMU KWA UNDANI PRODUCER S2KIZZY, KATIKA MAHOJIANO HAYA.

Share This
Wengi tunapenda kusikiliza Nyimbo mbalimbali na kuwapa sifa za kumwaga Wasanii na kuwasahau watu ambao pengine huwa na Mchango mkubwa kuzidi hata Msanii mwenyewe.
Kutana na Mtayarishaji wa Muziki ambae katika Muziki ameanza kufahamika siku za karibuni lakini kwa kazi aliyofanya mpaka sasa unaweza kusema alikuwepo katika Kiwanda cha Burudani kwa kipindi kirefu.

Mwandishi wetu, Alifanya mahojiano na mtayarishaji wa Muziki matata, S2KIZZY ambae anapatikana katika Studio ya Switch Records, Ambayo inamilikiwa na Msanii Quick Racka.

Wapi Ametokea?

Anafunguka kuwa safari yake ya Muziki ilianza tangu akiwa Shule Ya Msingi,Kiwira Coal Mining ambapo anasema alikuwa akipenda kuimba na pia kupiga ngoma na mambo mengine ya kiburudani.

“Nilikuwa napiga ngoma watu walikuwa wanapenda sana, na pia nilipomaliza Shule Ya Msingi nilianza kufuatilia mitandaoni namna watu mbalimbali wanavyotengeneza mabiti sababu tayari nilianza kuona kama ninaweza kufanya hicho kitu,”


“Mimi sijawahi kufundishwa kuandaa nyimbo, nilikuwa najifundisha mwenyewe kwa kuangalia namna watu mbalimbali wanafanya, Nashukuru sana kwa sapoti kwa Mwalimu wangu mkuu wa Shule ambae alikuwa na Studio ambayo mara kwa mara nilikuwa ninakaa pale na kujifunza,”

Ngoma kali zake anazozielewa.

Anasema kuwa mpaka sasa amefanya ngoma nyingi sana na Wasanii tofauti lakini mpaka sasa ngoma kama Rich Mavoko aliyomshirikisha Patoranking- Rudi, Country Boy aliyomshirikisha Mwana Fa-Turn Up na pia Country Boy-Ahaa Wapi ndizo anazozikubali zaidi na kuziheshimu.

“Ngoma ya kwanza kunipa zaidi mafanikio ni Ahaa Wapi ambayo nilifanya na Country Boy naiheshimu sana na pia hata ngoma zingine kam Jay Mo ngoma ya Me And You zipo nyingi sana ila hizo naziheshimu sana,” aliongeza

Nae pia kumbe ni Msanii.

Anafunguka zaidi kuwa watu pia wajue kuwa yeye pia ni Msanii lakini anasubiri wakati sahihi wa kuachia wimbo wake.
“Mpaka sasa nina Albamu kama nne hivi nasubiri wakati sahihi ili namimi nianze kuachia Nyimbo kama msanii na sio mtayarishaji wa Muziki pekee,”

Anamzungumziaje Country Boy?

“Yani kiufupi jamaa ana mchango mkubwa sana kwangu, sababu ndio mtu wa kwanza kuniamini na kufanya kazi na mimi, na baada ya kufanya nae kazi tu nilianza kuona njia nyingi zimeanza kufunguka mpaka sasa nipo hapa,” anasema

Kuhusu kazi za Kimataifa.

Anasema mpaka sasa kafanya kazi na wasanii wakubwa Afrika, kama Casper Nyovest,Nasty C, Patoranking pamoja na wasanii wengine.


“Hizo ngoma naimani kwa mwaka 2018 zinaweza kuachiwa kwahiyo tuendelee kusubiri watu wazidi kuona ufundi wangu mwingine nje kidogo ya Bongo,”

Mtayarishaji (Produza) Anaemkubali sana.

“Mimi namkubali sana  Nahreel, tangu muda sana nilikuwa namuangalia na kuna mengi nimejifunza kutoka kwake ila ndio mtayarishaji wangu ninaependa sana kazi zake,” anasema

Pesa yake ya kwanza alifanyia nini

“Pesa yangu ya kwanza aisee sikumbuki fresh kwa sababu pesa za utayarishaji mimi nimeanza kupata tangu nikiwa nasoma ila nakumbuka kwa asilimia kubwa nilikuwa nazitumia kununua vifaa mbalimbali vya Studio kama Headphones,Mics na vifaa vingine,”

“Ila mpaka sasa nashukuru Mungu Pesa kadhaa nilizopata nimeziingiza katika mambo mengine ya kibiashara zaidi si unajua tena hizi kazi zetu,” anaongeza


No comments:

Post a Comment

Pages