Baada ya kuachia singo yake ya Sauda mkali ambae alikuwa memba pia wa kundi la Ya Moto Bendi,Enock Bella Ameweka wazi kuwa ili kuifanya sauti yake kuwa nzito huwa anatumia pia baadhi vyakula kama Pili Pili na vinginevyo.
Akifunguka katika kipindi cha Leo Tena,Enock anasema anaweza kuimba sauti laini lakini inampa wakati mgumu sana hasa kutokana na vyakula anavyotumia ambavyo vinafanya sauti yake iwe nzito.
"Mimi natumia vitu kama Pili Pili yani vyakula ambavyo vinaharibu sauti kwangu ndo vinaenda fresh kabisa,na sifikiri kama nitakuja kubadirika kuimba kama sauti ya akina Beka sababu ninaweza lakini inanitesa sana," alisema
SOMA PIA:MAKOSA HUWEZI KUAMINI YALIFANYWA KATIKA FILAMU HIZI
Pia aliongeza kuwa mahusiano yake na memba wa kundi lao wapo fresh,na wanapeana sapoti huku akieleza kuwa kundi hilo bado lipo na ni wakati tu ukiwadia watu watawasikia tena kwa mara nyingine.
"Kundi bado lipo,ni wakati tu utawadia watu wataona ila kwa sasa tumeamua kila mmoja apambane na hali yake kwanza ili tutaona tu,"aliongeza
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Mhariri Pia Mwandishi Mkuu Katika Tovuti Hii, Usiache Kupitia Kila Siku Kwa Habari Moto Moto.
No comments:
Post a Comment