FAIZA ALLY AWAPONDA WAIGIZAJI, BAADA YA WASTARA KUOMBA MSAADA - teknomovies
FAIZA ALLY AWAPONDA WAIGIZAJI, BAADA YA WASTARA KUOMBA MSAADA

FAIZA ALLY AWAPONDA WAIGIZAJI, BAADA YA WASTARA KUOMBA MSAADA

Share This
Baada Ya Wastara kupost kuomba msaada kwa Rais Magufuli, pamoja na Makamu Wa Rais Mama Samia Suluhu na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda kuhusu kupata matibabu ya Mguu wake ambao umeanza kuharibika kutokana na kukosa pesa ya kwenda kufanya matibabu.

Mwanadada Faiza Ally ambae, Pia ni Mwigizaji amefunguka juu ya suala hilo huku akiwaponda wasanii hao wa maigizo kuwa hawana Ushirikiano huku akisema zaidi kuwa kwa hali ambayo kapata Wastara ingeweza hata ndani ya Wasanii wenyewe kutatuliwa.

"Najua sina umuhimu kwenye industry ya filamu kutokana kuna wenyewe wenye sanaa yao na ukubwa wao ktk secta hiyo lkn nimehuzuria kwenye vikao kazaa katika kujitia umuhimu wa uwepo wangu na kujiunga ktk magrupu yao ili niwe pamoja nao kama msanii mwenzao lkn Kuna hali flani ile kwamba wewe sio muhimu....na kwa kweli nimeamua kujitoa kwenye magrupu kwa sababu kiukweli hayatimizi malengo kiufupi zaidi ya kuchangia misiba. ..kitu ambacho sio kibaya lkn kikubwa zaidi nilichoona wasanii wa filamu ushamba. ..u mimi na ujinga unasumbua sana hata pale unapotoa mawazo mazuri hayachukuliwi uzito na hata yanapo chukulia ni nguvu za coca ...nazungumza haya kutoka na post ya msanii mkubwa kabisa kuomba msaada wa kutibiwa ni aibu. ..wasanii ni watu wakubwa sana ...wasanii wote mngekua na malengo na umoja mna uwezo wa kumsaidia msanii mwenzenu bila kuomba lkn umoja huo hamna kila mtu ni bora ya mwenzie...hivi mtaomba mpaka lini maana huyo sio wa kwanza na kwa mtindo huu hata kuwa wa mwisho kabisa! Basi nyinyi vikongwe mlio shikilia hii sanaa fanyeni kitu ..sikilizeni hata mawazo ya wasanii chipkizi tuwe na umoja flani wa kazi na kujisaidia kupitia sisi sisi ....maisha ya wasanii yanisikisha kutoka na nguvu walio nayo ni vitu tofauti sana ..yaani ni ile kuna mtu unatamani umjue lkn ukishamjua tu unajuta kumjua kutokana na ushamba na ujinga ulio mjaa. ..Jamani tunajua kwamba wasanii wengi duniani tumetokea kwenye maisha duni na elimu hatuna lkn tunayo nafasi ya kuiga na kujifunza mazuri ...ukisha kuwa star ukan"ga'ngania tu unayo yajua unakua mjinga JIFUNZENI MAARIFA MAPYA .....NYINYI HAMSTAHILI KUWA MASKINI KABISA !"
Post ya Faiza Ally
Post Ya Wastara


No comments:

Post a Comment

Pages