Tupac Kweli Ni Mzima,Tumuombe Radhi Chid Benz? - teknomovies
Tupac Kweli Ni Mzima,Tumuombe Radhi Chid Benz?

Tupac Kweli Ni Mzima,Tumuombe Radhi Chid Benz?

Share This

WIKI kadhaa zilizopita msanii mkongwe Chidi Benz alisikika akisema kuwa yupo kwenye mipango ya kufanya kolabo yake na Tupac. Alipoulizwa zaidi kwamba Tupac yuko wapi,kwa majibu yake alisema kuwa yupo Cuba.

Kutokana na kauli hiyo wengi waliichukua kama msanii huyo ameanza kuchanganyikiwa na kuanza tena kurudia matumizi ya unga pasipo kujua sio yeye pekee ambae anaamini Tupac yupo hai na sehemu wanayoamini kuwa yupo Cuba.

Nao vipi tunaweza kusema ni machizi? Ukiachana na hicho wanachokiamini pia wana sababu nzito ambazo huzitumia katika kuamini kwao.

Katika makala hii nimekuandalia baadhi ya sababu kadhaa ambazo zinafanya kifo cha Tupac kionekane kama ni uongo uongo na kuwa mshikaji yupo sehemu Fulani anakula kuku kwa mrija huku akiendelea kutucheki na wasanii wetu.


      
Mwili wake baada ya kufa.

Baada ya Tupac kupigwa risasi na kufariki mwaka 1996 mwili wake ulichofanyiwa ni kama wahindi wanavyofanya ulichomwa moto lakini baada ya tukio haukuwahi kuonekana tena.

Kiongozi wa lebo ya Death Row ambae siku ya kupigwa risasi kwa Tupac alikuwa nae pamoja , Suge Knight anasema “ mtu ambae alitakiwa kuchoma mwili wa tupac nilimpatia kiasi cha dola milioni tatu toka kwangu tena keshi, lakini kitu ninachokijua baada ya hapo ni sikuwahi msikia tena huyo jamaa au kumuona nilisikia alistaafu na kuondoka,”

“Huwa najiuliza Tupac kwa hili ni kweli alikufa, sasa yuko wapi,” aliongeza.

2.   Picha yake ya mwisho.

Tupac alipigwa risasi Septemba 7 mwaka 1996 huko Las Vegas. Lakini cha kushangaza kidogo picha yake ya mwisho iliyopatikana akiwa pamoja na Suge Knight ilikuwa imepigwa septemba 8 na kuzidi kuleta sintofahamu katika hilo suala.

3.       Makaveli



Katika albamu yake ya The Don Killumunati:The 7 Day Theory iliachiwa huku Tupac akijiita Makaveli.

Jina hilo alianza kujiita Pac likitokana na mwanafalsafa maarufu kutoka Italia ambae alikuwa akiamini katika kuigiza kifo kama njia ya kumpiga adui yako katika vita. Kimbembe ni kuwa picha ya albamu ilimuonesha rapa huyo akiwa katika msalaba na akiamini kuwa baada ya kifo chake angefufuka baada ya siku saba.

Na pia ukichukua neno Makaveli,kama ukilipangua unapata “Am alive.K.” Hapo ndio utata uzidi kwamba jamaa vipi kwani.

4.       Mistari Yake.

Kuna baadhi ya mistari yake ambayo iligusia kuhusu kifo chake hata kabla tukio halijatokea.

Katika wimbo wa “Ain’t hard 2 find” kuna mistari anasema “I heard rumor that I died ,murdered in cold blood traumatized/pictures of me in my final states-you know Mama cried . but that was fiction,some coward got the story twisted,” kwa tafsiri ya kwamba “Nimesikia watu wakiongea kwamba nimekufa,nimeuwawa kikatili kwa kuogofya,najiona katika nyakati zangu za mwisho na najua Mama unalia lakini hayo ni maigizo waoga wamegeuza stori,” hapo vipi kwanini watu wasiwe na mashaka na jamaa kwamba yupo hai?

     Albamu zake.

Hapa ndio watu hukosa zaidi majibu, baada ya kifo chake Albamu za Tupac tisa zimeweza kuachiwa na baada ya kifo umaarufu wake ulizidi maradufu. Swali linakuja alipata muda gani kurekodi nyimbo zote hizo za kuweza kukaa katika albamu tisa?

6.           Yupo Cuba?



Hapa labda ndio muanze kumuomba ladhi Chid Benz. Watu wanaamini kwamba dizaini Fulani yupo Cuba kisa ni kuwa ,Pac alikuwa na ukaribu sana na mwanaharakati Assata Shakur ambae inasemekana kuwa alikimbilia nchini Cuba.

Mwanamke huyo wa nguuv ambae mpaka sasa endapo atakanyaga ardhi ya Marekani basi hukumu yake itakuwa ni kifo hivyo aliamua kukimbilia Cuba ambako mpaka leo anaishi huko.
Kwa maana hiyo watu wanahisi itakuwa aliamua kuacha seke seke huku na kwenda kuungana na mwanaharakati huyo.

7       Video zake.

Katika video ya Toss it Up Tupac anaonekana akiwa amevaa snika ambazo hazikuwepo kipindi anakufa.
Pia kuna wanaosema katika video ya Live and Die in La wakati Tupac anaruka katika gari anaonekana akiwa amevaa snika za Michael Jordan ambazo hazikuwepo kwa kipindi hicho.

Vyanzo:Oxygen.com na mitandao mingine





No comments:

Post a Comment

Pages