YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-4 - teknomovies
YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-4

YAFAHAMU MAKUNDI MAWILI MAHASIMU YA HIP HOP NCHINI MAREKANI-4

Share This
Ilipoishia………….

Pamoja na visanga vyote hivyo Biggie hakutoa diss Track kujibu mapigo wala hakujibu lolote juu ya kile kilichoendelea aliendelea na mishe zake kama kawaida mpaka baadae alipokuja kuachia ngoma “Who shot ya” na hii aliichia baada ya kifo cha Tupac.

Endelea……………..

Ukimya wa Biggie juu ya beef hii uliwashtua wengi hasa mashabiki zake wakawa wanajiuliza kwa nini Biggie hamjibu Tupac? Kwa nini amekuwa kimya? Haoni kama hii itaathiri kazi zake kwani anashambuliwa bila yeye kurudisha mashambulizi? Hayo yalikuwa maswali waliokuwa wakijiuliza mashabiki wa Biggie. Pamoja na kutoonyesha reaction yoyote bado hili beef limebaki kwenye historia ya game ya hip hop duniani.


Kutokana na mwenendo huo mashabiki wakawa wanahoji ni nani aliyeshinda kwenye beef hili? Moja kwa moja credit ikamuangukia Tupac kwani mauzo ya kazi zake yaliongezeka huku ya Biggie yakishuka hivyo wakahitimisha mjadala kwa kusema Tupac ni mshindi (Tupac he won the feud)

Kwa kuwa Tupac aliuawa mwaka mmoja kabla ya Biggie, hivyo Biggie alitumia muda huo kuziba mianya aliyoachiwa na Tupac kwenye kazi zake . Kwa upande wangu pia ukiniuliza ni nani alishinda kwenye beef hii nitakujibu ni Tupac kwani jina la Tupac limeenea maeneo mengi duniani na pia amewahamasisha vijana wengi kwenye game ya rap ukilinganisha na Biggie na pia muziki wake unajulikana sana ukilinganisha na kazi za Biggie hivyo kwa upande wangu pia nithubutu kusema Tupac alishinda kwenye beef hii.


BIG Notorious
Swali lililopo vichwani mwa watu ni nani alimuua Tupac?

Zipo nadharia(Theories) nyingi juu ya kifo cha Tupac , ukumbuke Tupac ni mmoja ya wasanii waliouza sana sokoni, ameuza jumla ya rekodi 75 million, bila kusahau baadhi ya movie ambazo ali act na kuweka heshima kwenye jamii ya rap.

Tupac alipigwa risasi tareh 7 September 1996 huko Las Vegas Nevada baada ya mechi kati ya Mike Tyson na Bruce Seldon, Baada ya shambuli hilo alichukuliwa na kupelekwa katika hospitali ya chuo kikuu cha Tiba kwa ajili ya matibabu.

Alifanyiwa upasuaji kadhaa lakini kutokana na moyo wake kuathirika kwa kiasi kikubwa siku sita mbeleni yaani tarehe 13 September aliaga dunia.


Suge Knight
Baada ya kufariki mtu wa kwanza kunyooshewa kidole juu ya mauaji hayo ni Suge Knight , tofauti na inavyodhaniwa kuwa ni Biggie na Puff Daddy ambao hawa walidhaniwa kuhusika kwenye tukio la awali la Tupac kupigwa risasi akiwa studio, Sasa kwa nini Suge Knight amenyooshewa kidole yeye kuhusika na mauaji haya ? 

Itaendelea…………  


Usisahau kutufollow Instagram na Twitter @Teknomovies kwa Updates mbalimbali na pia Subscribe Youtube Channel ya DM Online Tv


Pages