Facebook Yafikisha Watembeleaji Bil 2 Kwa Mwezi. - teknomovies
Facebook Yafikisha Watembeleaji Bil 2 Kwa Mwezi.

Facebook Yafikisha Watembeleaji Bil 2 Kwa Mwezi.

Share This
Mtandao wa Facebook ndio unaoongoza katika mitandao ya kijamii. unaongoza kwa mambo yote kuanzia kuwa na watumiaji wengi na kuingiza mapato mengi kuliko mitandao mingine ya kijamii.

Kingine cha ajabu ni kwamba watanzania wengi wanazani kuwa mtandao huo umeishiwa kwamba hauna ishu tena lakini ukweli usiofichika ni kwamba mtandao huo bado upo kileleni.

Mmiliki na mkurugenzi wa kampuni hiyo ya Facebook,Mark Zuckerberg alizitoa taarifa hizo mwenyewe katika ukurasa wake katika mtandao huo.

Kingine ambacho kinaifanya facebook kuzidi kupata umaarufu ni vitu ambavyo viko ndani yake, kuanzia magroup, page za watu na biashara nyingi zinazofanyika
Kwa siku Facebook wapata like milioni mia nane katika post za watu tofauti tofauti, hivyo unaweza ona ni jinsi gani mtandao huo unavyotembelewa kwa siku.

Na kumbuka sio lazima kila kitu mtu atakachokiona ataki like.
Mark amesema kwa sasa Facebook haina wazo la kuunganisha watu duniani kama zamani bali sasa inataka kuwaweka karibu zaidi kuliko mwanzo.

Kutokana na kufikiwa na lengo hili la watumiaji bilioni mbili kwa mwezi Facebook kama kampuni imesema itaongeza viengele kibao katika mtandao huo na pia kutakua na video ya kuonyesha furaha yao kwa kufikia hapo.

Ningependa kusikia kutoka kwako niandikie hapo chini sehemu ya comment.

Source: Teknokona

Pages