Rasmi: Uzinduzi wa Iphone 8 Kufanyika Septemba 12 Mwaka Huu - teknomovies
Rasmi: Uzinduzi wa Iphone 8 Kufanyika Septemba 12 Mwaka Huu

Rasmi: Uzinduzi wa Iphone 8 Kufanyika Septemba 12 Mwaka Huu

Share This
Uzinduzi wa iPhone 8 kufanyika Septemba 12 mwaka huu
Baada ya tetesi nyingi za lini kampuni ya Apple itafanya uzinduzi wa iPhone 8, toleo la simu yake mpya sasa rasmi wamethibitisha kwamba uzinduzi utafanyika Septemba 12, 2017.

Uzinduzi huo utafanyika Huko Cupertino, California katika ukumbi wa Steve Jobs, ambapo ni mara ya kwanza kufanyika hapo kwa tukio kama hilo.

Tukio hilo la Septemba 12 mbali na iPhone 8 linatarajiwa kutangazwa kwa iPhone 7s, iPhone 7s Plus, Apple Watch 3 na 4k Apple TV.

Wakati uzinduzi wa iPhone 8 ukisubiriwa kwa hamu kubwa, sokoni tayari kuna Samsung Note 8 ambayo inategemewa kuleta usumbufu kwa mauzo ya iPhone 8.

Septemba 12 inaangaliwa kama siku ya Apple

Source:Teknokona

Pages