Mbinu Ambazo Huenda Huzijui Kutoka Google Play Store #Uchambuzi - teknomovies
Mbinu Ambazo Huenda Huzijui Kutoka Google Play Store #Uchambuzi

Mbinu Ambazo Huenda Huzijui Kutoka Google Play Store #Uchambuzi

Share This

google-play-logoGoogle play ni  moja kati ya Soko kubwa la kushuusha App nyingi za bure na za kununua. Soko hili hutumiawa na watumiaji wa vifaa vya Adroid japokua hata kwa kompyuta yako unaweza kuingia katika soko hili sema ni vigumu kushusha App. Google play ndio soko linaloongoza kwa App za bure ukiachana na masoko mengine kama lile la AppStore linalomilikiwa na Apple Inc.

Soko la Google Play kama jina lake lilivyo linamilikiwa na kampuni ya Google, sasa ili kujua mbinu tofauti kuhusiana na soko hili endelea kusoma zaidi
A: FUATILIA SIMU ILIYO POTEA AU KUIBIWA
Ndio unaweza kufuatilia simu yako iliyopotea au kuibiwa lakini simu yako ya Android inabidi iwe na vitu muhimu vitatu ambavyo ni
  • Kifaa chako kiwe kimeunganishwa na akaunti yako ya google
  • Kifaa chako lazima kiwe na uweza wa kuingia katika mtanadao (ineternet)
  • Lazima kifaa chako kiwe kimewasha sehemu ya ‘Location Settings’


Kama simu yako imekidhi hayo mambo yote hapo juu, basi tunaenda sawa. Sasa fungua mtandao wa ‘Android Device Manager‘ – https://www.google.com/android/devicemanager na kisha anza kufuatilia simu yako iliyopotea au kuibiwa ili kujua ipo eneo gani kwa kutumia ramani.
Muonekano wa Mtandao wa Android Device Manager Pale unapoitafuta Simu Yako. Inakuonesha Ilipo na Inakupa uwezo wa Kubeep!
Muonekano wa Mtandao wa Android Device Manager Pale unapoitafuta Simu Yako. Inakuonesha Ilipo na Inakupa uwezo wa Kubeep, kuilock – funga, na pia kuifuta data zako.

B: FUTA DATA ZAKO ZOTE KWA KUTUMIA GOOGLE PLAY
Hii ni moja kati ya zile mbinu nzuri tuu unazoweza fanya ukiwa na kifaa chako cha Android.  Kwa kutumia njia hii unaweza uka RESET skifaa/simu yako ya android lakini kifaa hiko lazima kiwe na mambo mawili ya muhimu
  • Hakikisha kina uweza wa kimtandao (internet)
  • Hakikisha kifaa chako kimeunganishwa na akaunti ya google
Kama una uhakika kifaa chako kimekidhi mambo yote hayo basi nenda katika ‘Android Device Manger‘ kisha futa kila kitu katika simu yako iliyoibiwa au kupotea. Hii itahakikisha usalama wa vitu vyako (mfano Picha, nyaraka, video na mafaili mengine ya muhimu) ndani ya kifaa.  Kwa Njia 3 za Ku Reset simu ya Android soma Hapa

C: RUDISHIWA KIASI ULICHOTUMIA KUNUNUA APP USIYOIPENDA

Hivi umenunua App ambayo baadae haifanyi kazi kama ulivyodhani au hukuipenda na akajuta kupoteza hela yako bure?.  Sasa unafanyaje?

Google hurudisha kiasi ulichotumia kwa App ambazo hazifanyi kazi kama ulivyotegemea lakini kwa zoezi hili kukamilika kuna vigezo na masharti ambayo inabidi yazingatiwe.. zoezi hili litafanyika mara moja tuu kwa kila App hivyo usije kujisumbua kuomba kurudishiwa kiasu chako zaidi ya mara moja. 

Kitu kingine ni kwamba unaweza omba kurudishia kiasi chako baada ya masaa mawili kupita tangia ulivyo nunua App hiyo.  Ili kurudishiwa kiasi chako, fungua Google play store na itafute hiyo App ya kulipia uliyoishusha. Ikishatokea ataona sehemu imeandikwa ‘REFUND’ bofya juu yake na Google ita rudisha kiasi hicho ndani ya masaa 48. Kitu kingine kizuri kuhusu hii ni kwamba hakuna sera ya maswali kwa hiyo unaweza omba kurudishiwa kiasi chako. Hii inamaanisha huwezi kuulizwa maswali mia ili kurudishiwa kiasi chako.



D: PATA ORODHA YA APP ZAKO ZA ZAMANI
Umeuza kifaa chako cha Android hivi karibuni na unataka orodha ya App ulizokuwa unatumia hapo awali? Google inakusaidi katika hilo, ‘Sign In’ katika Google Play kwa kutumia Akaunti yako ya kwanza kisha nenda  Apps > My Apps ili kupata orodha ya App zako zote ulizowahi kushusha kwa sababu google inahifadhi App zote ulizowahi shusha
Eneo la 'My Apps' ktk Google Play
Eneo la ‘My Apps’ ktk Google Play

Je una mbinu nyingine yeyote akilini kuhusiana na Google Play store ?  basi usisite kutuambia sehemu ya komenti hapo chini, pia usisahau kusambaza makala hii. 

Pages