Ifahamu Miji Ambayo Ni Hatari Zaidi Kuishi - teknomovies
Ifahamu Miji Ambayo Ni Hatari Zaidi Kuishi

Ifahamu Miji Ambayo Ni Hatari Zaidi Kuishi

Share This
Hatari ipo karibu nasi wakati wote, ajali pia nazo tuko nazo ingawa tunaskia kwa nadra, lakini watu wameuawa bila kutarajia kwa kupigwa risasi, mafuriko, na hata kuzama! Kisha kuna hatari za ndani, kama kasoro za moyo ambayo inaweza kuua mtu kwa papo, au labda ubongo kupata hitilafu. 

Ni ukweli kabisa hakuna njia maalum iliyopo kwa ajili yetu ili kuepuka baadhi ya hatari ya maisha, lakini sisi tunaweza kufanya ajali na hatari zipungue kutokana na matendo yetu. Nimekuwekea list ya miji hatari zaidi duniani.

1. Aleppo, Syria

Dunia nzima inafahamu hali ya kisiasa nchini Syria mapigano ya kijeshi ni kawaida . Wakazi wengi wa Aleppo wanaishi maisha kama wakimbizi, na wamekimbilia juu ya mpaka katika nchi jirani ya Uturuki kama hali itaendelea kuwa mbaya zaidi.Mbali na mapigano, maisha ya kila siku pia ni magumu zaidi kutokana na ukosefu wa mahitaji ya msingi kama vile umeme na maji, ambavyo ni mara kwa mara kuvurugika au kukatwa kabisa.

2. San Pedro Sula, Honduras

Hakuna shaka kwamba Honduras inapokea wageni wengi wa kitalii kutokana na hali yake ya kuvutia na ya kitropiki . Uhalifu unafanyika sana katika maeneo ya San Pedro Sula, na watalii mara nyingi ni waathirika wa utekaji nyara na uhalifu mwingine wa kifedha na  mara nyingi kuja na mwisho kusikitisha sana .San Pedro Sula ina bahati mbaya ya kuwa mji mkuu unaongoza kwa mauaji dunia nzima.

3. Caracas, Venezuela

Kifo cha Rais Hugo Chavez mwaka 2013 imeonekana kama ni matokeo ya kuongezeka kwa uasi katika mji mkuu wa Nchi hiyo. Wananchi mara nyingi wanaingia mtaani kuandamana kutokana na kushinikiza serikali iliyopo idhibiti masuala ya rushwa na pia huripotiwa vifo vya wananchi mara kwa mar. Vikundi vya kihalifu vinaongezeka siku hadi siku hali inayopelekea ukosefu wa amani.

4. Cape Town, South Africa

Cape Town inafurahi kwa sasa kupunguzla kwa kiasi idadi ya vitendo vya kihalifu kwa muongo mmoja sasa lakini jambo hilo halitaribiki kutokana na idadi kubwa ya wahamiaji wanaoingia mjini humo.
Usishangae  ukifika Cape town na kukuta dawa za kulevya zikiuzwa km njugu hyo ndio tabia ya mji huo na inakadiriwa ni zaidi ya 14% ya vijana huongezeka kila mwaka ktk matumizi ya dawa za kulevya. Vipo vikundi vinavyojihusisha na uhalifu hadi kuvunja milango na kuingia majumbani kisha kupora na kujeruhi na muda kuuwa kabisa .


5. Kabul, Afghanistan
Afghanistan ni nchi yenye vita kwa wakati wote majeshi ya magharibi yamepiga kambi hapo kusambaratisha vikosi vya kigaidi kama Al- shabaab. Kujiua kwa mabomu (kujitoa mhanga) ni kawaida sana kuskia kwani ni km desturi. Hili ni eneo hatari zaidi katika mataifa ya Asia. Maeneo mengine ni kama Acapulco, Mexico, Mogadishu, Somalia, Karachi, Pakistan







No comments:

Post a Comment

Pages